HEADER AD

HEADER AD

TWAJIVUNIA TANZANIA, TWAJIVUNIA KUWA WATANZANIA


NCHI yetu ya thamani, kwa jina ni Tanzania,

Jina lake la thamani, twapenda kulisikia

Nchi inatuthamini, na inatujali pia

Twaipenda Tanzania nchi yetu ya thamani


Tuna mbuga za wanyama, serengeti na manyara

Wapo pia kina duma, na wale kina sungura

 Twaipenda Tanzania nchi tuliyozaliwa

Tunayo pia milima,  Tanzania inang'ara

Twaipenda Tanzania nchi yetu ya thamani


Mabonde twajivunia, hakika yanavutia,

Maua yanachanua, asali twajipatia

Maua yananukia, porini yameenea

Twaipenda Tanzania nchi yetu ya thamani


Tanzania yapendeza, wa nchi waitamani

Kwa amani yaongoza, ulaya na duniani,

Ninapenda kuwajuza, Tanzania ya thamani

Twaipenda Tanzania nchi yetu ya thamani


Mlima wenye thamani, ni mrefu Afrika

Wasikika duniani, kwa urefu si utani

Kilimanjaro jamani,  mlima twauthamini

Twaipenda Tanzania nchi yetu ya thamani


Bendera inapepea, amani kuashiria

Rangi zake zavutia, kijani na njano pia

Nyeusi twajivua, ni sisi Watanzania

Twaipenda Tanzania nchi yetu ya thamani


Kituoni nimefika, hongera Watanzania,

Twajivunia hakika, nchi yetu Tanzania

Twaishi bila mashaka, nchi tunajivunia

Twaipenda Tanzania nchi yetu ya thamani


Kutoka Kilimanjaro Tanzania

Najivunia kuwa Mtanzania

SirDody Dody Kilimanjaro

0762396923 au

0675654955

No comments