HEADER AD

HEADER AD

DKT. MOLLEL : TANZANIA KWA SASA HAINA MGONJWA MPYA WA MARBURG


Na Alodia Dominick, Biharamulo 

Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel, amesema, Tanzania kwa sasa haina mgonjwa mpya wala mhisiwa wa ugonjwa wa Marburg, watu wawili wa familia moja waliokuwa na ugonjwa huo wamepoteza maisha.

Dkt. Mollel akiwa mkoani Kagera Januari 28, 2025 amesema jitihada za Serikali zinazoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuimarisha sekta ya afya kwa kushirikiana na wadau mbalimbali zimesaidia kufanikisha mapambano dhidi ya ugonjwa huo.

     Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel akizungumza na Waandishi wa habari.

Dkt Mollel amesema tangu Rais alipotangaza uwepo wa marburg, watu 281 walihisiwa kuwa na maambukizi ya virusi vya marburg ambapo watu wawili wamepoteza maisha.

Amesema watu 145 kati ya wahisiwa wote waliwekwa chini ya uangalizi katika vituo mbalimbali vya kutolea huduma baada ya kusambaa kwa ugonjwa  huo katika Wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera.

Kutokana na taarifa ya Wizara ya Afya watu hao 145 wameruhusiwa kuungana na familia zao baada ya wataalam wa afya kujiridhisha kuwa hawana maambikizi ya virusi hivyo.

 "Mpaka sasa watu wawili wa familia moja wamepoteza maisha huku Wahisiwa  44 wakiendelea kuwekwa chini ya ungalizi wa wataalam wa Afya wakiwa majumbani" amesema Dkt. Mollel 

Amesema  wahisiwa 92 wanaendelea na uangalizi katika kambi mbalinbali za kutolea huduma za afya kwa kufanya uchunguzi mbalimbali na kujua hali zao zinaendeleaje ndani ya siku  ya siku 21.

Amesema kwa kushirikiana na Mashirika ya kimataifa na Wahudumu wa Afya ngazi ya jamii  tayari Kaya 10,892 wamepatiwa Elimu ya kujikinga huku vitu o vya   ukaguzi wa abiria wanaotoka nchi mbalimbali vikiongezeka kutoka vituo 8 Hadi 11 ambapo kwa siku abria 8,000 hadi 10,000 wanapimwa hali zao.

Mollel ametoa wito kwa wananchi kuendelea kuchukua tahadhari kwa kufuata sheria zinazotolewa na wizara ya afya  ili kuendelea kukinga afya zao bila kuathiri uchumi wao .

Amesema serikali inaendelea  kuchukua hatua za haraka juu ya  maswala ya magonjwa ya milipuko na kuhakikisha  familia na jamii za wahisiwa na wote walioko katika kambi wanapata huduma zinazostahiki ili kuwa chini ya uangalizi bila wasiwasi.

"Nawapongeza wataalam wetu kwa kuchukua hatua za haraka  mlizofanya na mnaendelea  kutoa huduma katika jamii , ugonjwa huu ni hatari  na wananchi wanatakiwa kuchukua tahadhari , kwa kuwa hatua za kujikinga ziko wazi basi wanaweza kuendelea na shughuli zao huku wakijikinga"amesema Dkt Mollel .

Mkurugenzi wa kinga toka Wizara ya Afya Dk.Ntuli Kapologwe ameyataja mashirika ya kimataifa yanayoendelea kutoa huduma kwa huko Biharamulo kuwa ni  WHO, UNICEF na CDC ambao wanaendelea kisaidia serikali katika mapambano ya ugonjwa huo mpaka sasa.

Amesema serikali kwa kushirikiana na wataalamu wa  Afya wameondoa hofu katika jamii na shughuli , zinaendelea kama kawaida  huku wakiwa na furaha kuwa hawqjapata kesi mpya ya mgonjwa wa Marburg.



No comments