BILIONEA MAARUFU DUNIANI AGA KHAN AMEFARIKI AKIWA NA UMRI WA MIAKA 88
BILIONEA maarufu duniani na kiongozi wa kiroho wa dhehebu la Ismaili katika dini ya Kiislamu, Aga Khan, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 88.
Mzaliwa huyo wa Sweden, aliyekuwa na uraia wa Uingereza na Ureno, alianzisha miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwemo hospitali na shule kwa lengo la kuwasaidia, watu wa kawaida, katika nchi za afrika na bara Asia.

Aga Khan wa nne, ambaye jina lake halisi ni Mwanamfalme Karim Al-Hussaini, ameombolezwa na viongozi mbalimbali kama mfanyabiashara na tajiri aliyegusa maisha ya watu.
Maisha yake ya utotoni aliishi nchini Kenya na baadaye akaenda Tanzania kuendeleza biashara za babu yake mwaka 1957 katika nchi hizi mbili, alizowekeza pakubwa.
Rais wa Kenya William Ruto na Suluhu Hassan wa Tanzania, wameomboleza kifo chake na kumsifia kwa mchango na uwekezaji wake mkubwa katika sekta ya elimu na afya katika nchi zao.
Naye, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, amemwelezea Aga Khan kama nembo ya amani, aliyehubiri mshikamo na kukariri kuwa dini ya Kiislamu.
Post a Comment