MIKONONI MWA MANESI - 1
.jpg)
MIKONONI mwa manesi, wengi wetu tumepita,
Mikononi mwa manesi, uhai tulipopata,
Mikononi mwa manesi, na hawakutupepeta,
Wauguzi na manesi, mbarikiwe na Mungu.
Mikononi mwenu sisi, wengi ndimo tulipita,
Wa jadi pia manesi, sifa hizi wazipata,
Mlitutunza manesi, hadi sasa tunapeta,
Wauguzi na manesi, mbarikiwe na Mungu.
Mikononi mwa manesi, huduma tunazipata,
Nyingi bila ukakasi, hatuhitaji kusuta,
Mwawajibika manesi, tunapoipatapata,
Wauguzi na manesi, mbarikiwe na Mungu.
Kinamama na manesi, mkono vidole pata,
Hasa kukiwa nafasi, ya watoto kuwapata,
Wapatana na manesi, furaha waweze pata,
Wauguzi na manesi, mbarikiwe na Mungu.
Tunapopata nafasi, huko tunapitapita,
Tukiwaona manesi, tutambue wakipita,
Wametuzalisha sisi, ndio sasa tunapeta,
Wauguzi na manesi, mbarikiwe na Mungu.
Kibidi kuwe nafasi, na Mungu wetu kuteta,
Alinde wetu manesi, huduma tuzidi pata,
Wasiipate mikosi, tukabaki twatepeta,
Wauguzi na manesi, mbarikiwe na Mungu.
Wako wachache manesi, sio wengi hao hata,
Watumiao nafasi, kutuacha tunasota,
Kila tukiita nesi, wao wajivutavuta,
Wauguzi na manesi, mbarikiwe na Mungu.
Nyie wachache manesi, kazi njema mmepata,
Kutuhudumia sisi, afya zikisitasita,
Tunawapenda manesi, maombi yetu mwapata,
Wauguzi na manesi, mbarikiwe na Mungu.
Hivyo jueni manesi, thawabu mtaipata,
Kazi yenu kwetu sisi, kwa Mungu heri mwapata,
Tusaidie manesi, afya tuweze kupata,
Wauguzi na manesi, mbarikiwe na Mungu.
Na haki zenu manesi, twafurahi mkipata,
Hizo zipande kwa kasi, mpate bila matata,
Nyumbani kuwe msosi, mijengo muweze pata,
Wauguzi na manesi, mbarikiwe na Mungu.
Na Lwaga Mwambande (KiMPAB)
lwagha@gmail.com 0767223602
𝗜𝗝𝗨𝗪𝗘 𝗧𝗛𝗔𝗠𝗔𝗡𝗜 𝗡𝗔 𝗡𝗚𝗨𝗩𝗨 𝗬𝗔 𝗣𝗘𝗦𝗔 𝗜𝗟𝗜𝗬𝗢 𝗡𝗗𝗔𝗡𝗜 𝗬𝗔𝗞𝗢.
ReplyDeleteMtu mwenye pesa
akijiskia vibaya atakumbuka mali zake
atarudi kwenye hali ya kawaida,
Ukikosa pesa ni mapambano na ni ngumu kurudi kwenye hali ya kawaida.
Watu wanasema hakuna thamani ya pesa au mali inayo zidi thamani ya mtu.Hata wewe ni zaidi ya mali na pesa.
Kujiskia vizuri ni high frequency kujiskia vibaya ni low frequency.
Ukiishi kwenye high frequency riziki zinafunguka
Ukiishi kwenye low frequency riziki zinafunga.
Mtu mwenye pesa atakumbuka mali zake. Atarudi hali ya kawaida, Hali ya kujiskia vizuri
Ipo kauli inasema aliye nacho huongezewa.watu hawa wanadumu kwenye high frequency.
High Frequency ndio channeli ya riziki.
Muda wote ukiwa kwenye high frequency nyota inang'aa bila kulazimishwa.
Muda wote ukiwa kwenye low frequency nyota inazima bila kulazimishwa.
Asikudanganye Mtu kwamba huna kitu.
Wewe umepewa muda hapa duniani ujitambue ili uwe wewe. Ndio maana bado unaishi.
Kujiskia vizuri ni channeli ya Riziki.
Hakikisha unapatikana kwenye channeli hiyo.
Riziki zitakuona ukiwa kwenye high frequency.
Low frequency ni barabara ya giza na mikosi hakuna riziki kwenye mikosi.
Huna pesa tafuta nyaraka iliyo andika wewe ni nani.
Utakumbuka wewe ni nani.
Itakusaidia kujiskia vizuri.
Wachawi wana kauli zao , nini kina mpa kiburi. Watu wabaya wanapenda ujiskie vibaya muda wote.
Ili uendelee kuwa masikini.
Muda wowote ukijiskia vibaya. shika nyaraka Yako,
iliyo andika wewe ni nani,
mara zote ukiisoma uta kumbuka uwezo wako mkubwa .
utajiskia vizuri,
kwa kuwa uwezo wako ni
hazina ya siri.
(Kwanza kabisa nataka kukwambia kwamba hakika utajiri ni hazina kutoka kwa mwenyezi Mungu na pia kuna viumbe alio wapa mamlaka na nguvu ya kumiliki mali)
CALL/WHATSUP +255 742162843
MPAKA MASAA 48(SIKU2) PAPO HAPO KWA MASHARTI MAALUM KIKUBWA UWE MWAMINIFU, JASILI NA UWE NA UTAYARI WA KUPOKEA MASHARTI YA KUTUNZA SIRI HII SIO MZAHA......
KUMBUKA MALIPO NI BAADA YA KUFANIKIWA
kwa maelezo kamili piga namba +255742162843
(KWANINI USUMBUKE,HACHA KUTANGATANGA, NA MAISHA NI MAFUPI PUUZA UONGOFU WA KUWA MTU KUWA TAJIRI NI DHAMBI WAKATI AKUAMBIAE YEYE NI TAJIRI (Tumia ufahamu kujinasuaUTAJIRI WA NDAGU(MASHARTI) NDANI YA MASAA 72(SIKU TATU) PAPO HAPO KIKUBWA UWE MWAMINIFU, JASILI NA UWE NA UTAYARI WA KUPOKEA MASHARTI YA KUTUNZA SIRI HII SIO MZAHA......
POPOTE ULIPO TIBA INAKUFIKIA HATA WALIO NJE YA NCHI
#kenya
#Uganda
#Congo
#Rwanda
#Burundi
#tanzania #trendingpost
KARIBU DOKTA MDIRO
NIPIGIE/ WHATSUP
+255 742162843