HEADER AD

HEADER AD

MWANDISHI WA HABARI ALIYEKAMATWA AACHIWA HURU NA KUREJESHEWA VIFAA VYAKE VYA KAZI


Anaandika Edwin Soko, Mwanza

MWANDISHI mwenzetu Daud Julius mmiliki wa chombo cha habari cha mtandaoni Tarime TV, aliyeachiwa kwa dhamana jana kituo kikuu cha polisi Mwanza yuko huru na amerejeshewa vifaa vyake vya kazi. 

Jana majira ya saa tatu usiku Daud aliachiwa kwa dhamana baada ya kukamatwa na askari Polisi kutoka Mwanza waliomfuta wilayani Tarime na kumleta mwanza akituhumiwa kwa kosa la matumizi mabaya ya mtandao.

Leo majira ya saa 4:00 Asubuhi alirudi kuripoti kituoni akiwa na wakili wake tuliyempatia kwa msaada zaidi.

            Mwenyekiti wa chama cha Waandishi wa habari mkoa wa Mwanza, Edwin Soko.

Baada ya kuripoti ameachiwa huru bila kuwa na kesi yoyote ya kujibu . Mlalamikaji kwenye tuhuma hizo amethibitisha kuwa Mwandishi huyo hakuhusika kwenye kupiga picha na kusambaza clip hiyo.

Pia Daud amepewa vifaa vyake vyote vilivyoshikiliwa  na Polisi.

Ahsanteni wote kwa umoja na mshikamano tulioutoa tangu kukamatwa kwa mwenzetu.

>> Ilivyokuwa kabla ya kuachiwa huru

Mwandishi wa Habari Daud Julius akamatwa na Jeshi la Polisi

Nimepokea taarifa ya kukamatwa kwa Mwandishi wa Habari Daud Julius (Tarime TV), na Jeshi la Polisi Tarime, Mkoa wa Mara  mchana wa leo Jumapili, Agosti 9, 2026 

Nimeongea na Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa kiwezesha waandishi wa habari Tarime, Helena  Magabe amethibitisha kukamatwa kwa mwandishi huyo.

       Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa kiwezesha waandishi wa habari Tarime, Helena  Magabe kulia akiwa na Mwandishi wa habari Daud Julius aliyekuwa amekamatwa na Polisi Mwanza.

Baada ya kukamatwa David Julius na Polisi walianza safari ya kusafirishwa na Polisi kuelekea Mkoa wa Mwanza.

Sababu za kukamatwa kwake na Jeshi la Polisi  haijawekwa wazi  hadi sasa.

Kwa sasa tunaendelea kufuatilia kujua sababu za kukamatwa kwake, hivyo tuendelee kuwa na subira wakati tunafuatilia.

Tunaliomba Jeshi la polisi liweke wazi sababu za kukamatwa kwake.

>> Apewa dhamana 

MWANDISHI wa habari  Daud Julius maarufu King Davy wa Tarime TV, toka Tarime, Mkoa wa Mara  ambaye nilitoa taarifa ya kukamatwa kwake Tarime na kusafirishwa kuja Mwanza, usiku huu baada ya kufikishwa Mwanza amepata dhamana.

Usiku huu nimefanya mazungumzo na RCO wa Mwanza na ambaye alitoa maelekezo kama kuna mtu wa kumdhamini aweze kumdhamini .

Nimefanikiwa kumtuma mwanachama wetu wa MPC na MISA  Tanzania  Maganga Gwesega kwa ajili ya kumdhamini mwenzetu na tumefanikiwa amepata dhamana mida ya saa tatu usiku.

Tuhuma za kosa ni matumizi mabaya ya mitandao kwa kusambaza clip ya video ya maamuzi ya kesi ya mahakamani, hivyo atarudi kuripoti kesho( leo) Agosti 10, 2026 .

Binafsi namshukuru sana RCO Mwanza kwa ushirikiano wake, Pia Maganga Gwesaga.

Tunawashukuru wote kwa ushirikiano wenu ambapo kwa sasa Daud yuko huru kuendelea na majukumu yake. 

Imetolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa habari mkoa wa Mwanza , Edwin Soko.




No comments