HEADER AD

HEADER AD

KARIBUNI AL-WAFAA ENGLISH MEDIUM ISLAMIC PRIMARY SCHOOL NA AL- WAFAA ISLAMIC SEKONDARY SCHOOL_....

Singida imeshamiri, kwa shule nyingi hakika

Zinatamba kwa uzuri, vizuri zinasikika,

Zinayo mengi mazuri, ninawatoa mashaka,

Lakini Al- Wafaa ni shule bora zaidi


Al- Wafaa yasifika, kwa mazingira mazuri,

Yanavutia hakika, nayasema siyo siri,

Maua yamepambika, yananukia vizuri,

Lakini Al- Wafaa ni shule bora zaidi


Mabweni yakuvutia, watoto wafurahia,

Kwa ndani yanavutia, hata na kwa nje pia,

Nidhamu yazingatia, maadili na tabia,

Lakini Al-Wafaa ni shule bora zaidi


Za sayansi maabara, shule inajivunia,

Hakika zina ubora, kwa viwango zavutia,

Vifaa vyake imara, na tena vinavutia,

Lakini Al-Wafaa ni shule bora zaidi


Watoto inawalea, kwa dini kuzingatia,

Kiimani wanakua, tena kwa njema tabia,

Watoto inapokea, kwa sifa kuzingatia,

Lakini Al-Wafaa ni shule bora zaidi


Elimu mbili hutoa, ya mazingira na dini,

Vigezo huzingatia, vya kutoka wizarani,

Shule inajivunia, elimu yenye thamani,

Lakini Al- Wafaa ni shule bora zaidi


Ina walimu mahiri, tena waliobobea,

Wanafundisha vizuri, kwa vitabu kurejea,

Kwa kufundisha hodari, kila mbinu hutumia,

Lakini Al-Wafaa ni shule bora zaidi


Ni shule yenye thamani, kwa elimu kuthamini,

Inasifika nchini, kwa kushinda mitihani,

Inashinda mitihani, ya kitaifa na ndani,

Lakini Al-Wafaa ni shule bora zaidi


Namaliza kuandika, yale nilokusudia,

Mengi nimeyaandika, kwa shairi kupitia,

Shule imethibitika, kwa elimu kuitoa,

Lakini Al-Wafaa ni shule bora zaidi


Mtunzi Sirdody Dody

0724917212

_Kilimanjaro_

No comments